Tuesday, July 25, 2017


Mwenyekiti wa Taasisi ya Dodoma youth development organization (DOYODO) akiwakilisha katika kupokea mfano wa hundi iliyotolewa kwa vikundi mbalimbali ikiwemo DOYODO ilipokea mkopo rasmi zilikabiziwa na Naibu Waziri wa Tamisemi Mhe Selemani Jafo na Mkulugezi wa Manispaa ya Dodoma

Thursday, July 20, 2017

picha za ziara ya shule ya msingi mlimwa c










Mwenyekiti wa Taasisi ya vijana mkoa wa Dodoma DOYODO hakiwa kwenye ziara ya kutembelea shule ya msingi Mlimwa c katika harakati za kutatua changamoto za wanafunzi ikiwemo Maji na zoezi la kugawa vitabu kwa wanafunzi pia Taasisi ya DOYODO kwa kushilikiana na wadau wa Elimu iliweza kuchangia pesa kwajili ya kuvuta Maji shilingi 475,000 na mifuko kumi ya cement kwajili ya ujenzi Taasisi inaendelea kumuunga mkono mh Rais wa jamuhuri wa mungano wa Tanzania kazi za Taasisi ni kusaidia kusukuma Maendeleo

Sunday, July 16, 2017

Taasisi ya Vijana ya DOYODO kufanya ziara shule ya msingi mlimwa C

Taasisi ya vijana mkoa wa Dodoma "DODOMA YOUTH DEVELOPMENT ORGANIZATION (DOYODO) inatarajia kufanya ziara siku ya jumatano tarehe 19/07/2017 ikiongozana na afisa elimu wa manispaa ya Dodoma, Afisa mtendaji na wadau wengine wa maendeleo kutembelea shule ya msingi mlimwa c iliyopo kata ya miyuji Wilaya ya dodoma mjini kusikiliza changamoto mbalimbali za wanafunzi ikiwemo maji na kujaribu kuzitatua

Wednesday, July 5, 2017

Naibu waziri wa Tamisemi awapa pongeza taasisi ya vijana DOYODO kwa harakati zake

Mwenyekiti wa taasisi ya DODOMA YOUTH DEVELOPMENT ORGANIZATION (DOYODO) akiwa na naibu waziri wa tamisemi Mhe Seleman Jafo ofisini kwake. Pia mhe naibu waziri alipata nafasi ya kuzungumza na wanataasisi na kutoa pongezi zake za dhati kwa jitihada zinazoonyeshwa na Taasisi ya DOYODO.

Sunday, July 2, 2017

TANGAZO....Nafasi za kujitolea katika taasisi ya vijana ya DOYODO


Taasisi ya vijana mkoa wa Dodoma (DOYODO) inatakaza nafasi za mabalozi kumi (10) wa kujitolea katika shughuli za kijamii kuanzia leo tarehe 02/07/2017 mpaka tarehe 06/07/2017 hivyo ukiwa kama kijana unayependa maendeleo ya kijamii kielimu na kiuchumi ni fursa ya kuomba kwa kutuma barua ikiwa imeambataniswa na CV katika email yetu doyodoorg2@gmail.com

Sunday, June 25, 2017

Kiongozi wa mwenge wa uhuru asisitiza kukuza umuhimu wa viwanda kukuza uchumi


kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa amesisitiza kushiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu" Piga vita rushwa, ukimwi, malaria na madawa ya kulevya. Amewapongeza sana vijana wa DOYODO katika kukuza maendeleo ya vijana kiuchumi kielimu na kijamii

Vijana wa Doyodo wakiwa katika msafara wa kupokea mwenge wa uhuru


Vijana wa taasisi ya vijana ya DOYODO walijitokeza kupokea mwenge wa uhuru maeneo ya veyula wenye kauli mbiu isemayo "Shiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu" Piga vita rushwa, ukimwi, malaria na madawa ya kulevya.

Mwenyekiti wa Taasisi ya vijana Mr Rajabu Juma N'hunga akipokea mwenge wa uhuru

Mwenyekiti wa taasisi ya vijana ya DOYODO akipokea mwenge wa uhuru wenye kauli mbiu "shiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu"

Friday, June 23, 2017

Naibu waziri Mhe Seleman Jafo akagua mradi wa Elimu unaofanywa na vijana wa DOYODO









 

 Naibu waziri wa ofisi ya raisi tawala za mikoa na serikali (TAMISEMI) Mhe Seleman Said Jafo akipata maelezo kuhusu mradi wa elimu na pia kutoa maelekezo katika ziara ya kuwatembelea vijana wa Dodoma Youth development organization (DOYODO)

Naibu waziri Mhe Seleman Jafo akagua mradi wa matofali Unaofanywa na vijana wa DOYODO




Naibu waziri wa ofisi ya raisi tawala za mikoa na serikali (TAMISEMI) Mhe Seleman Said Jafo akijaribu kufyatua matofali katika ziara ya kuwatembelea vijana wa Dodoma Youth development organization (DOYODO)

Naibu waziri wa TAMISEMI Mhe Seleman said Jafo atembelea Taasisi ya vijana DOYODO




Naibu waziri wa ofisi ya raisi tawala za mikoa na serikali (TAMISEMI) Mhe Seleman Saidi Jafo akiwa katika ziara ya kuwatembelea vijana wa Dodoma Youth development organization (DOYODO)